Rais Museveni ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Mashariki amefanya ziara ya siku moja ya kikazi nchini.

Rais Museveni akizungumza na wanahabari mara baada ya kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Dkt. Magufuli, alieleza kuwa lengo la ziara hiyo ni kumpa taarifa Rais Magufuli kuhusu masuala yanayojiri kwenye mkutano wa BRICS uliofanyika Afrika Kusini.

Katika mkutano huo  ambao Afrika Mashariki ilishiriki kama kanda, Rais Museveni alitumia nafasi hiyo kuzishawishi nchi wanachama wa BRICS kuja kuwekeza Afrika Mashariki katika sekta za miundombinu ya uchukuzi na viwanda.

Aidha, Rais Museveni amempongeza Rais Magufuli kwa jitihada zake za kufufua Shirika la ndege la Tanzani ambalo litaleta mchango mkubwa katika kukuza utalii nchini.